Ijumaa, 19 Februari 2016

SHULE KUMI BORA KITAIFA KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE

Baraza la mitihani Tanzania limetangaza matokeo ya mtihani wa kidato cha nnewamwaka2015 yanayoonesha kiwango cha ufaulu kushuka kwa asilimia 0.80. 
Akitangaza matokeo hayo, Katibu Mtendaji wa Baraza hilo Dkt Charles Msonde amesemakuwa jumla watahiniwa 272,947 sawa na 67.53% ya watahiniwa wote waliofanya mtihaniwa kidato cha nne 2015 wamefaulu tofauti na mwaka 2014 amba ufaulu ulikuwa 68.33%. 
Msonde amesema kwa upande wa watahiniwa wa shule, waliofaulu ni 240,996 sawa na asilimia 67.91 ya waliofanya mtihani, wasichana wakiwa 11,125 (64.84) na wavulana wakiwa 124,871 (71.09).

Hakuna maoni: